Mbunge wa Viti Maalum, Fatma Toufiq
Kauli hiyo ameito hii leo Mei 12, 2021, Bungeni Dodoma, wakati akichangia hoja ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa hii leo na Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Dorothy Gwajima.
"Kundi kubwa ambalo linaonesha lipo kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa Ukimwi ni watoto wenye umri wa miaka 14-24, na katika wale vijana 10 wanaoopimwa watoto wa kike 8 ndiyo wanaombukizwa sana, nilikuwa nashauri akina Baba ebu muwaonee huruma hawa watoto, sababu mmeacha kuwafuata akina mama watu wazima mnawafuata hawa watoto", amesema Mbunge Fatma
Aidha ameongeza kuwa "Hebu waacheni hawa watoto wasome watimize malengo yao, haya mambukizi mapya hawa watoto wanayapata kwa akina Baba ambao hawajapima".