Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Toeni maoni ya kuboresha mitaala- Prof. Ndalichako

Friday , 18th Jun , 2021

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, ametoa wito kwa wadau wa elimu waliojitokeza katika mkutano wa kupokea maoni ya kuboresha mitaala nchini, kutoa maoni yatakayojikita kuwajengea wahitimu ujuzi na stadi zitakazoweshe kujitegemea.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam Prof. Ndalichako amesema ni matarajio kuwa maoni yatakayopatikana kutoka kwa wadau mbalimbali yatasaidia kujibu changamoto ya wahitimu kumaliza kisha kusubiria matangazo ya kazi badala ya kujiajiri wenyewe.

"Wadau wamekuwa na wito kuwa na mitaala ya kuwaandaa vijana kujitegemea kujiajairi au kuajiriwa, ni imani yangu kuwa kupitia mkutano huu mtatoa maoni na mapendekezo yanayolenga kujibu changamoto hii pia suala hili tuliwekee mkazo kwa sababu ni kilo cha wadau kuwa wahitimu wanamaliza wanasubiri tu matangazo ya kazi," amesema Prof. Ndalichako.

Awali akizungumza Prof. Ndalichako amesema serikali imejikita katika kujenga uchumi wa viwanda hivyo kuna budi kuwa na wahitimu wabunifu watakosaidi kukuza uchumi wa nchi.

"Tumejikita katika kujenga uchumi wa viwanda, lazima tuzalishe wahitimu wabunifu wa waweze kubuni vyanzo zaidi vya kukuza na kuimarisha uchumi wa taifa, taifa lisilo na wahitimu mahiri kamwe haliwezi kusonga mbele," amesema Prof. Ndalichako.

Aidha, Prof. Ndalichako amaeto wito kwa taasisi za elimu ya juu nchini kuendesha mijadala ya kupitia mitaala kwani itawasaidia kukusanya maoni na kuyafanyia maboresho.

"Nitoe wito kwa taasisi za elimu ya juu nchini waanzishe mijadala kama hii, na kupata maoni kwa wadau mjielekeeze kushirikiana na taasisi binafsi muweze kujua mataraijio ya wahatimu ili nanyi kuingia kazini kutazama kwa kina," amesema Prof Ndalichako.

Leo Prof. Ndalichako alikuwa mgeni rasmi katika mkutano wa kupokea maoni ya wadau kuhusu uboreshaji wa mitaala ya elimu ya awali, msingi na sekondari ulioandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania nchini (TET).
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa