Monday , 16th Aug , 2021

Kesi ya kupinga tozo za miamala ya simu iliyofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) leo Agosti 16, 2021, itatajwa tena kwa mara ya pili katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga

Taarifa ya kesi hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga, na kueleza kuwa kesi hiyo ilifunguliwa Julai 27 mwaka huu.

Tozo ya uzalendo katika miamala ya simu kwa mtumaji ama mpokeaji wa pesa zilianza kutozwa Julai 15 mwaka huu, na tayari serikali iliahidi kulishughulikia suala hilo baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi.