Tuesday , 31st Aug , 2021

Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi (Mahakama ya Mafisadi), itatoa uamuzi Septemba 1, 2021 kama ina/haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi na Ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe na wenzake.

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe

Hilo limeelezwa leo kesi hiyo ilipotajwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Elinaza Luvanda.

Katika kesi hiyo upande wa washtakiwa ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala uliibua hoja ya kutaka kesi hiyo ifutwe kutokana na Mahakama ya Mafisadi kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi za Ugaidi.

Aidha kwa upande wa Jamhuri ulipinga hoja hiyo na kusema Mahakama hiyo ina mamlaka.