
Mbunge wa kuteuliwa Humphrey Polepole
Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 3, 2021, Jijini Dodoma, wakati alipoitikia wito wa Kamati ya Maadili ya Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ambayo imemuita lakini haikubainishwa wazi sababu zilizopelekea Mbunge huyo kuitwa mbele ya kamati hiyo.
"Kikao cha maadili ni kikao cha ndani, kwahiyo taarifa zote zitatoka kwa utaratibu wa chama," amesema Mbunge Polepole.
Wabunge wengine walioitwa kufika mbele ya kamati hiyo ni Mbunge wa Ukonga Jerry Silaa na Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima.