Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasaan
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro, mara baada ya mkutano wake maalum na wawekezaji kutoka nchi ya Bulgaria uliofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo wameahidi kujenga hoteli zenye hadhi ya nyota tano kwenye hifadhi 4 za Taifa ambazo ni Kempinski Serengeti, Kempinski Manyara, Kempinski Tarangile na Kempinski Ngorongoro.
''Juhudi kubwa za kimkakati za Royal Tour zilizoendeshwa na Rais wetu zimeweza kuzaa matunda ambapo leo tumepokea wawekezaji mahiri kutoka Bara la Ulaya ambao watawekeza kwenye hoteli kwa kujenga hoteli tatu za nyota tano za 'brand' ya Kempinski kwa uwekezaji wa Dola za Kimarekani Milioni 72," amesema Dkt Ndumbaro
Waziri Dkt. Ndumbaro ameongeza kuwa, ujenzi huo ni mkubwa na unakadiriwa kuanza rasmi mwezi Januari 2022 ambapo amemshukuru Rais Samia kwa kuwezesha kuwapigia 'pass' na wao kupitia Wizara ya Maliasili ni utekelezaji ikiwemo kupokea wawekezaji.