Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

DC Shinyanga aipokea timu ya Namthamini

Monday , 27th Sep , 2021

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko ameipokea timu ya East Africa TV na East Africa Radio ambayo ipo wilayani humo kwaajili ya kugawa taulo za kike kwa wanafunzi kupitia kampeni ya Namthamini.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko

Mboneka ameeleza kuwa ni kweli kumekuwa na changamoto ya wanafunzi wa kike waliofika katika umri wa hedhi kutofika shuleni kwa kukosa taulo za kike hivyo ameishukuru East Africa TV, East Africa Radio pamoja na Flaviana Matata Foundation.

Aidha Jasinta Mboneko amesema kuna fursa kubwa ya watu kuwekeza wilayani humo hususani kwenye sekta ya uchimbaji madini hivyo anawakaribisha wawekezaji wengi wa ndani ambapo pia ujenzi wa uwanja wa ndege ukikamilika kutakuwa na fursa nyingi zaidi kwenye viwanda.

Wafanyakazi wa East Africa TV na East Africa Radio wakiwa na mkuu wa Wilaya ya Shinya Jasinta Mboneko (katikati)

''Huko nyuma tulikuwa na tatizo kubwa sana ila tumekuwa tukiwaelekeza walimu wakuu na wakuu wa shule kuhakikisha kila mwezi mara mbili mara tatu kuzungumza na watoto wa kike kuhusu hedhi salama na namna ya kujitunza na hii imechangia mimba za utotoni kupungua,'' ameeleza DC Jasinta.

Wafanyakazi wa East Africa TV na East Africa Radio wakiwa na mkuu wa Wilaya ya Shinya Jasinta Mboneko (katikati)

Ameongeza kuwa, ''hizi taulo za kike zimekuwa zikisaidia watoto wa kike kutokosa masomo katika wilaya yetu maana unakuta mtoto anakosa masomo takribani siku 5 kwa mwezi sasa ukipiga hesabu ni siku nyingi sana na anakosa vipindi vingi sana''.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto