Friday , 25th Feb , 2022

Michuano ya wazi ya Mexico (Mexican Open) imeingia hatua ya nusu fainali ambapo nyota kutoka nchini Urusi Daniil Medvedev atacheza dhidi ya Mhispania Rafael Nadal kwenye nusu fainali ya kwanza na mchezo huo ukikumbushia mchezo wa fainali wa michuano ya wazi ya Australian 2022.

Nyota wa tennis Daniil Medvedev

Medvedev mwenye umri wa miaka 26, alimuondoa Mjapan Yoshihito Nishioka kwa seti 2-0 ( 6-2 6-3) huku jumatatu nyota huyo akitarajiwa kushika nafasi ya kwanza kwa viwango vya ubora duniani baada ya nyota raia kutoka Serbia  Novak Djokovic kuondolewa ambaye  alipoteza  mbele ya raia wa Czech Jiri Vesely  mjini Dubai.

"sio rahisi kucheza mchezo huku ukipokea taarifa nzuri za kwenda kuwa nafasi ya kwanza kwa ubora duniani ingawaje  lengo la kwanza ilikuwa kushinda kwa kila mchezo na kufanya vizuri"amesema Medvedev

Upande wa Nadal mwenye umri wa miaka 35 ambaye alitwaa taji la Grand Slam la 21 mjini Melbourne yeye alitinga hatua ya nusu fainali baada ya kumfunga Muingereza Tommy Paul kwa seti  6-0, 7-6 (7-5) huku nusu fainali ya pili itawakutanisha Muingereza  Cameron Norrie atakayecheza na Mgiriki Stefanos Tsitsipas.