Monday , 28th Feb , 2022

Rais wa Brazil, Jair Bolsonaro amekataa kuiwekea vikwazo Urusi baada ya kuvamia ardhi ya Ukraine na kuanzisha vita, na kusema Brazil haitaegemea upande wowote kuhusiana na kile kinachoendelea Ukraine.

Rais wa Brazil, Jair Bolsonaro

Bolsonaro ameikosoa Ukraine kwa kusema walimwamini mchekeshaji katika kuamua hatima ya nchi, akimaanisha kumuamini Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ambaye zamani alikuwa mchekeshaji.

Brazil inategemea mbolea kutoka Urusi na kumuwekea vikwazo italeta madhara makubwa kwenye kilimo nchini Brazil.