
Mtakwimu Mkuu wa serikali ya Tanzania Dkt.Albina Chuwa, na Meneja Mradi kutoka Ofisi ya Takwimu ya Korea Kusini ,Charlie Seo, wakisaini mikataba hiyo
Makubaliano hayo yamesainiwa mkoani Iringa na Mtakwimu Mkuu wa serikali ya Tanzania Dkt.Albina Chuwa, na Meneja Mradi kutoka Ofisi ya Takwimu ya Korea Kusini ,Charlie Seo kwenye mafunzo kwa walimu wa Sensa ya Watu na Makazi ya 2022.
Kwa kupitia ushirikiano huo NBS watapatiwa mafunzo katika nyanja mbalimbali ndani ya nchi na nchi ya Korea Kusini.