
Mfalme Zumaridi akiwa Mahakamani
Ombi hilo la Mawakili wa upande limewasilishwa hii leo Juni 17, 2022, ambapo Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Monica Ndyekobora, akawataka Mawakili hao kufikisha malalamiko hayo kwa uongozi wa Gereza Kuu la Butimba kwa ajili ya hatua zaidi huku akiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 30 ya mwezi huu.
Mfalme Zumaridi pamoja na wenzake wanakabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali na imeanza kutolewa ushahidi ambapo leo hii shahidi namba moja ametoa ushahidi mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mwanza.