
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar Salum Mwalimu
Kauli hiyo ameitoa hii leo Juni 23, 2022, jijini Dar es Salaam, wakati akiichambua bajeti ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
"Maisha yetu Wazanzibar ni Eid, ni moja kati ya matukio makubwa sana na tumezoea kununuliana nguo wakati wa sikukuu ya Eid, Wazanzibar tulikuwa hatuijui mitumba, mitumba labda tukija huku tukiiona ndiyo tunanunua, miaka hii miwili watoto wa Kizanzibar sikukuu ya Eid wanavaa mitumba, nguo hazishikiki,"amesema Mwalimu