Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uchimbaji madini maeneo ya hifadhi

Sunday , 3rd Jul , 2022

Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa maeneo yaliyopo kwenye hifadhi bado yanatafutiwa ufumbuzi ili wachimbaji wa madini waweze kuchimba na kunufaika na rasilimali hizo.

Dkt. Biteko amesema hayo alipotembelea na kuzungumza na wachimbaji wadogo katika eneo la Lugelele wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya katika ziara yenye lengo ya kukagua shughuli za uchimbaji madini na kutatua changamoto zinazowakabili wachimbaji hao wa madini ya dhahabu.

Ameongeza kuwa, Serikali inayatafutia ufumbuzi maeneo yaliyopo kwenye hifadhi ili kuwawezesha wachimbaji na hivyo kunufaika na rasilimali madini.

Amefafanua kuwa, maeneo yaliyopo chini ya Hifadhi ya Taifa (TANAPA) bado hayaruhisiwi kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo hayo mpaka sasa. Aidha, kwenye hifadhi za misitu amefafanuwa kuwa, Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) haijazuia shughuli za uchimbaji madini.

"Maeneo ya hifadhi ya wanyamapori hakuruhusiwi shughuli za kibinadamu, za uchimbaji madini zinazoruhusiwa ni za aina mbili tu, kutafiti mafuta na gesi na kuchimba madini ya nishati," amesisitiza Dkt.Biteko.

Ameongeza kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anataka kuwaona wachimbaji wanapewa fursa kwenye uchimbaji wa madini ili waweze kunufaika na rasilimali madini.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune amesema kuwa, shughuli za uchimbaji madini katika wilaya hiyo zimekuwa fursa kwa wananchi katika kujipatia kipato cha kila siku.

Amesema, wachimbaji wengi wanapata ajira katika maeneo hayo na amemweleza Waziri Biteko kuwa, wilaya ya Mbarali inapata wastani wa kilo 2.5 ya dhahabu ambayo huchangia kwenye Pato la Taifa na halmashauri hiyo.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ametembelea kiwanda cha kuzalisha kokoto cha TAZARA Kongolo Quarry ili kujionea shughuli zinazofanyika katika kiwanda hicho.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ