Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bidhaa za misitu lazima zipigwe chapa - Waziri

Monday , 4th Jul , 2022

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana, amewataka watengenezaji wote wa bidhaa za misitu nchini wahakikishe kuwa wanaweka alama inayoonesha bidhaa zao  zimetengenezwa Tanzania yaani "Made in Tanzania" ili bidhaa hizo zijulikane kuwa zimetengenezwa Tanzania.

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana

Balozi Dkt.Balozi Pindi Chana ametoa kauli hiyo wilayani Mufindi wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea kiwanda cha Dazhong Hood, kinachozalisha bidhaa zinazotokana na misitu na kubaini kuwa bidhaa zinazozalishwa na kiwanda hicho hazina alama inayoonesha kuwa zimetengenezwa Tanzania.

Waziri Chana amemtaka mmiliki wa kiwanda hicho Bw. Wu Bing ambaye ni raia kutoka China atekeleze agizo hilo na azingatie sheria, kanuni na taratibu za Tanzania. 

Mbali na agizo hilo Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana amepongeza juhudi za uhifadhi wa misitu nchini zinazofanywa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  na kuitaka taasisi hiyo  ieendelee kushirikiana na halmashauri za wilaya, wadau mbalimbali na wananchi katika jukumu la kuhifadhi misitu, kusimamia viwanda vya bidhaa zinazotokana na misitu ziwe na alama inayo onesha kuwa zimetengenezewa nchini Tanzania.

Kwa upande wake Mbunge wa Mafinga Mjini Mhe. Cosato Chumi amesema  sekta ya misitu ina mchango mkubwa kwa wananchi hasa wa Mafinga kwa kutoa  ajira nyingi na mchango mkubwa kwenye Mapato ya Halmashauri hiyo kwa asilimia 60,  hivyo yeye kama mwakilishi wa wananchi ataendelea kushirikiana  na Wizara katika uhifadhi wa Maliasili hiyo.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala