Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serengeti Girls kuanza na Japan Oktoba 12

Thursday , 28th Jul , 2022

Timu ya taifa ya wanawake chini ya miaka 17 ya Tanzania ‘Serengeti Girls’ imepangwa kuanza na Japan kwenye michuano ya Kombe la Dunia, itakayoanza Oktoba 11, mwaka huu nchini India.

Timu ya taifa ya wanawake chini ya miaka 17 ‘Serengeti Girls’

Serengeti Girls imepangwa kundi D na itacheza na Japan Oktoba 12 kwenye Uwanja wa Pardit Jawaharlal, jijini Nehru.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Morocco itacheza mechi ya ufunguzi dhidi ya Brazil kwenye Uwanja wa Kalinga Oktoba 11.

Serengeti Gils ambayo tayari imeingia kambini kujiandaa na michuano hiyo, itacheza mchezo wa pili Oktoba 15 dhidi ya Ufaransa kabla ya Oktoba 18 kumaliza dhidi ya Canada kwenye Uwanja wa DY Patil.

Tanzania sasa imeungana na Morocco na Nigeria kuiwakilisha Afrika na kukamilisha idadi ya timu 16 zitakazoshiriki fainali hizo za Dunia kati ya Oktoba 11-30 mwaka huu katika miji mitatu ya India zikiwa ni fainali za saba tangu michuano hiyo ilipoasisiwa mwaka 2008.

Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufuzu fainali hizo kwa timu za soka. Hadi kufuzu, Serengeti ilizing’oa Botswana, Burundi na kumalizia kwa kuitoa Cameroon baada ya kuibuka na ushindi wa jumla wa mabao 5-1.

 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi