Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Omanyala ashinda dhahabu Jumuiya ya Madola

Thursday , 4th Aug , 2022

Mwanariadha wa Kenya wa mbio fupi za mita mia moja Ferdinand Omanyala ameushangaza ulimwengu baada ya kuibuka mshindi na kutwaa medali ya dhahabu katika michezo ya nchi za Jumuiya ya Madola inayoendelea mjini Birmingham nchini Uingereza.

Ferdinand Omanyala mwanariadha wa Kenya- mbio fupi za mita mia moja.

Omanyala alimaliza mbio hizo kwa kumia muda wa sekunde kumi na nukta mbili na kuipatia Kenya medali ya kwanza ya dhahabu katika michuano hiyo baada ya kumshinda bingwa mtetezi wa mbio hizo Akani Simbine kutoka Afrika Kusini aliyemaliza katika nafasi ya pili.

(Bondia wa Tanzania Yusuf Changalawe (kulia) akinyanyuliwa mkono juu baada ya kushinda pambano)

Upande mwingine Tanzania imejihakikishia medali ya pili kwenye michuano hiyo baada ya bondia Yusuf Changalawe kumchapa kwa knockout bondia Arthur Langlier wa St. Lucia na kutinga nusu fainali kwenye mchezo wa ngumi za ridhaa za uzani wa juu wa kati (light heavyweight).

Kwa maana hiyo hata kama Changalawe atapoteza pambano la nusu fainali, bado atatunukiwa medali shaba kwa mujibu na kanuni za ngumi za ridhaa, kwani kanuni zao zinawatambua mabondia walioshindwa kwenye nusu fainali kuwa ni washindi watatu, huku wale walioshinda wataingia fainali ili kupata bingwa na mshindi wa pili.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja