Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

KMC FC yaifuata Namungo Ruangwa na wachezaji 20

Thursday , 29th Sep , 2022

Kikosi cha wachezaji 20 , Viongozi pamoja na Benchi la ufundi kimeondoka leo Jijini Dar es Salaam kuelekea Ruangwa mkoani Lindi kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC soka Tanzania Bara dhidi ya Namungo utakaochezwa siku ya Jumamosi Oktoba 1 katika uwanja wa Majaliwa.

Kikosi hicho cha Wana Kino Boys kimeondoka mapema leo kikiwa tayari kimefanya maandalizi ya kutosha kuwakabili Namungo ambapo itakuwa ugenini kwenye mchezo huo.

KMC FC chini ya Kocha Mkuu Thierry Hitimana inatambua ushindani wa mchezo huo na kwamba kila kitu kimekamilika tangu Timu ikiwa Jijini Dar es salaam wachezaji wote wako tayari kwa mchezo huo.

Katika msafara huo KMC FC imeacha wachezaji saba ambapo wote hawana changamoto yoyote na kwamba wataendelea kufanya mazoezi binafsi kulingana na programu ya Kocha Hitimana kwa ajili ya kujiandaa na mchezo mwingine unaokuja Oktoba saba dhidi ya Ruvu Shooting.

"Tunakwenda kwenye mechi yenye ushindani, lakini tumejipanga vizuri, tunawafahamu vizuri Namungo, licha ya ushindani kuwa mkubwa lakini kama Timu tunakwenda kwa tahadhari Ili kuhakikisha kwamba tunapata ushindi.

Kwa upande wa hali za wachezaji wote wameondoka wakiwa salama, wanahali  nzuri, wanamorali zaidi ya kutafuta ushindi kwenye mchezo huo muhimu, mashabiki na Watanzania wote ambao sikuzote wanaisapoti Timu ni jukumu la kila mmoja kuwaombea wachezaji afya njema ili kuhakikisha burudani ambayo wameonesha kwenye michezo minne iliyopita inaendelea dhidi ya Namungo. 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala