Tuesday , 4th Oct , 2022

Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA), Athumani Amasi, amewataka wasimamizi wa mitihadi ya darasa la saba inayoanza kesho Oktoba 5, kuhakikisha wanalinda haki ya watahiniwa hasa wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia mitihani yenye maandishi ya nukta nundu kwa wenye uono hafifu.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA), Athumani Amasi,

Na kwamba watahiniwa wote wenye mahitaji maalum waongezewe muda wa dakika ishirini (20) kwa kila saa kwa somo la Hisabati na dakika kumi (10) kwa kila saa kwa masomo mengine.

Aidha, amewaonya wamiliki wa shule binafsi na waratibu elimu, kutojihusisha na udanganyifu wa mitihani na kuwataka polisi walioko kwenye vituo vya mitihani kutoingia kwenye vyumba hivyo isipokuwa kama kuna dharura.