Tuesday , 1st Nov , 2022

Mamlaka nchini Nigeria zinasema nchi hiyo iko katika hatari kubwa ya kuingizwa kwa virusi vya Ebola kufuatia mlipuko wa ugonjwa huo nchini Uganda.

Nchi hiyo ya Afrika Magharibi haifungamani mpaka wa pamoja na Uganda.

 Hata hivyo, Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha Nigeria (NCDC) kinasema kiwango cha juu cha hatari kwa nchi hiyo kinatokana na "kiwango kikubwa cha usafiri wa anga kati ya Nigeria na Uganda na kuchanganya abiria, hasa katika vituo vya usafiri vya mikoa ya Nairobi, Addis Ababa na Kigali".

 

Mamlaka za afya zinasema ziko katika hali ya tahadhari, huku hatua kadhaa zikiwekwa "kuzuia na kupunguza athari za uwezekano wa mlipuko wa Ebola nchini Nigeria".

Hatua hizo ni pamoja na kuongezeka kwa ufuatiliaji na uchunguzi wa abiria katika viwanja vya ndege.