Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Milioni 470 zapotea jimboni kwa Mpina

Monday , 28th Nov , 2022

Waziri wa TAMISEMI, Angellah Kairuki, ameagiza TAKUKURU kuchunguza matumizi ya shilingi milioni 470, zilizotolewa na serikali kujenga shule mpya ya Sekondari Mwanduitinje, iliyopo jimbo la kisesa wilaya ya Meatu, ambapo fedha hizo zimeisha kabla ya mradi kumalizika ujenzi wake.

Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina

Waziri Kairuki ametoa agizo hilo baada ya kufika shuleni hapo akiwa katika ziara yake ya kikazi, ambapo Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mwita Joram, aliiomba serikali nyongeza ya fedha shilingi milioni 264 ili kukamilisha mradi huo, hali iliyoonesha kumshtua Waziri huyo na kuagiza uchunguzi ufanyike haraka ndani ya siku saba kubaini kama kuna ufisadi.

"Tunachotaka majengo haya yakamilike, hatuwezi tukawa tumemwaga hela yote halafu tukayaacha hivi, ndiyo maana nikasema hebu Afisa wetu wa TAKUKURU aingie kazini kwa siku saba na nitaomba hiyo ripoti inayojitegemea, halafu na Mkaguzi wetu Mkuu wa Ndani na yeye pia aweze kufanya uchunguzi ," ameagiza Waziri wa TAMISEMI.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina, amesema mkwamo wa mradi huo unawaathiri wanafunzi wanaotembea umbali wa kilomita 17 kwenda shuleni, hivyo ni muhimu hatua za haraka zichukuliwe ili Januari 2023, shule hiyo ianze kazi mara moja.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi