Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi TZ yamrejesha Zahera Ligi kuu

Friday , 2nd Dec , 2022

Aliyewahi kuwa kocha wa zamani wa Yanga, Mwinyi Zahera raia wa Congo DR amejiunga na klabu ya Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro kuwa kocha mkuu baada ya kufikia makubaliano na uongozi wa timu hiyo.

Zahera ambaye alikuwa mkurugenzi wa kukuza soka la vijana Yanga, amejiunga na timu hiyo leo akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Joslin Bipfubusa raia wa Burundi ambaye mkataba wake ulisitishwa Oktoba 26, 2022 kutokana na mwenendo mbaya wa matokeo, miezi mitatu tangu ajiunge nayo Julai 26.

Ikiwa chini ya Mrundi huyo, Polisi Tanzania ilicheza mechi tisa ikiambulia pointi tano tu baada ya kushinda moja, sare mbili na kufungwa sita, ambapo alitimuliwa baada ya kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Tanzania Prisons.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma ya klabu hiyo ambayo imechapishwa kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, makubaliano hayo yamefikiwa leo Desemba 2, 2022 mkoani Kilimanjaro baada ya mazungumzo ya muda mrefu na tahmini ya kina ya kuhitaji kufanya vizuri.

Taarifa hiyo ambayo imetolewa Afisa habari wa klabu hiyo, Frank Lukwaro imewaomba mashabiki na wadau kumpa ushirikiano kocha huyo katika kuliongoza benchi la ufundi.

"Klabu ya Polisi Tanzania inapenda kuujulisha umma na mashabiki wake  kuwa imefikia makubaliano na ndugu Mwinyi Zahera kuwa kocha Mkuu wa timu yetu,"

"Makubaliano na kocha Zahera yamefikiwa leo (Ijumaa) mkoani Kilimanjaro baada ya mazungumzo ya muda mrefu pamoja na tathmini ya kina kwa lengo la kufanya vizuri. Tunawaomba mashabiki na wadau wote kumpa ushirikiano Kocha Zahera katika majukumu yake," imesema taarifa hiyo.

Baada ya kuondolewa Bipfubusa, Polisi Tanzania ilikuwa chini ya Kocha John Tamba ambaye ameiongoza katika michezo mitano ya Ligi Kuu akishinda mmoja dhisi ya Ihefu, sare na Dodoma Jiji na kupoteza dhidi ya Singida Big Stars, Mtibwa Sugar na Simba.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa