Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maadhimisho ya sekta binafsi 2022 Tanzania yafana

Sunday , 4th Dec , 2022

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa wamiliki wa kampuni na taasisi binafsi nchini kuhamasisha na kuzipatia uzoefu kampuni zinazochipukia (business startups) ili kuongeza wigo wa Sekta Binafsi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango

Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya sekta binafsi 2022 nchini Tanzaniailiofanyika Masaki Jijini Dar es salaam.

Amesema Serikali imedhamiria kufanya kazi na Sekta Binafsi katika miradi mbalimbali ya ubia kama vile ujenzi wa barabara, miradi ya umwagiliaji na uzalishaji wa nishati hivyo ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na TPSF kukaa pamoja na kuangalia namna ya kuongeza ushiriki wa Sekta hiyo katika miradi ya ubia ili kukabiliana na mwitikio mdogo uliopo.

Pia Makamu wa Rais amesema bado Sekta Binafsi haifanyi vizuri katika kuchangamkia fursa mbalimbali na rasilimali za kimataifa katika kulinda mazingira.

Amewasisitiza wadau wote wa Sekta Binafsi chini ya TPSF kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, na Ofisi za Ubalozi kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuchangamkia rasilimali fedha za kulinda mazingira kama vile biashara ya hewa ukaa na Green Climate Fund kuibua miradi ya utunzaji wa mazingira ikiwa pamoja na utengenezaji wa nishati mbadala, viwanda vya kuchakata taka ngumu na miradi mingine ya aina hiyo.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa