Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapambano dhidi ya ujangili kuendelea - Serikali

Thursday , 8th Dec , 2022

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imesema itaendelea kuongeza nguvu katika jitihada za Kuzuia na Kupambana na ujangili wa wanyamapori na Biashara ya nyara na mazao ya misitu ili kutokomeza kabisa vitendo hivyo vinavyoathiri taswira ya nchi, uchumi na maendeleo ya uhifadhi

Hayo yamebainishwa leo jijini Arusha wakati wa ufunguzi wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wenyeviti wa Kamati za Kanda za Kiikolojia za Kuratibu Doria (TCG's) katika kukabiliana na ujangili na Biashara haramu ya wanyamapori nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Msaidizi wa Uzuiaji Ujangili na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi Taifa cha Kuzuia na Kupambana na Ujangili nchini Bw. Robert Mande , Afisa Wanyamapori Mkuu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. John Ngowi amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mafunzo na doria ili kuhakikisha majangili wanaokamatwa wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Amesema mkakati uliopo katika mapambano dhidi ya ujangili ni kuona watuhumiwa wote wanaokamatwa wanafikishwa mahakamani na mashauri yao yanaendeshwa haraka na kwa ufanisi ili adhabu inayostahili iweze kutolewa kulingana na matakwa ya sheria.

“Lengo la kutolewa kwa mafunzo haya ni kuharakisha na kuhakikisha majangili wote wanaokamatwa wanafikishwa mahakamani na mashauri yao yanaendeshwa kwa haraka na kwa ufanisi ili wahusika wapewe adhabu inayostahili kulingana na matakwa ya sheria za nchi yetu” Amesisitiza.

Amesema ujangili unaathiri ustawi wa jamii na kudumaza uchumi wa nchi hivyo  mafunzo hayo yatawasaidia Wenyeviti hao kupanga mikakati endelevu ya kukabiliana na ujangili huku akibainisha kuwa mitandao ya uhalifu wa rasilimali hizo wakati mwingine huanzia nje ya nchi ikihusisha watu wengi katika ngazi mbalimbali na inafadhiliwa na watu wenye uwezo mkubwa wa kifedha.

'' Ni imani yangu kuwa baada ya mafunzo haya wananchi wataanza kuona majangili wanachukuliwa hatua kali za kisheria zinazostahili.  Wataanza kuogopa kushiriki katika  vitendo vya ujangili'' Amesema Afisa Wanyamapori Mkuu, Ngowi

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatasaidia Watendaji wa Idara na Taasisi zinazohusika na ulinzi na uhifadhi wa wanyamapori na mazao ya misitu kupanga mikakati endelevu ya kukabiliana na ujangili hapa nchini pamoja na kuimarisha dhana ya umoja inayowezesha Idara na Taasisi za ulinzi wa wanyamapori na misitu kufanya kazi kwa pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Kupambana na Ujangili na Usafirshaji haramu wa Nyara, Theotimos Rwegasira amesema mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Duniani (UNDP) na Shirika la Mazingira (GEF) yatasaidia kupunguza ujangili kwa kiwango kikubwa.

 Amesema mafunzo hayo yatakayohitimishwa leo yanatarajiwa kuleta mafanikio makubwa katika vita dhidi ya ujangili ikiwa ni mwendelezo kuunga juhudi mkono juhudi za serikali za kukabiliana na ujangili.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ