Sunday , 11th Dec , 2022

Zaidi ya wananchi 2000 kutoka vijiji mbalimbali katika Halmashauri ya wilaya ya Chalinze mkoani Pwani, wamepatiwa matibabu ya magonjwa mbalimbali ikiwemo sukari, upasuaji wa mtoto wa jicho pamoja na kupatiwa miwani kufuatia kambi ya matibabu inayoendeshwa katika hospitali ya Msoga.

Mmoja wa wananchi waliopatiwa huduma

Wakizungumza baada ya kupatiwa matibabu baadhi ya wagonjwa wakiwemo wale waliofanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho wamepongeza kazi kubwa inayofanywa na madaktari hao kutokana na afya zao kuanza kuimarika.

Mratibu wa zoezi hilo Ragib Hasanal pamoja na Mganga Mkuu wa hospitali ya Msoga Dkt. Allen Mlekwa, akielezea ujio wa madaktari hao utakavyosaidia kupunguza adha ya wagonjwa waliokua wakihitaji matibabu ya kibingwa.