
Wilbroad Mutafungwa, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza
Hayo yamebainishwa katika kikao maalum cha kuweka mikakati ya namna ya kukabiliana na uhalifu kilichowakutanisha wamiliki wa makampuni ya ulinzi na wamiliki wa vituo vya mafuta jijini Mwanza ambapo Kamanda wa Polisi mkoani humo Wilbroad Mutafungwa, akawataka kuhakikisha wanawatengea muda walinzi wao ili waweze kupewa mafunzo maalum ya utayari yatakayowasaidia kupambana kikamilifu na wahalifu
"Unakuta mlinzi wa kampuni analinda sehemu, akitokea mtu anafanya uhalifu basi mlinzi ndiyo anakuwa wa kwanza kukimbia, nawaagiza wamiliki wa makampuni ya ulinzi kuhakikisha wanawatoa walinzi wao ili wapate mafunzo ya utayari kutoka jeshi la polisi ili na wao waweze kufanya shughuli zao vizuri na kuacha kujihusisha na uhalifu," amesema Kamanda Mutafungwa
Katika hatua nyingine Kamanda Mutafungwa akawataka wamiliki wa vituo vya mafuta kuhakikisha wanafunga kamera kwenye vituo vyao ili pindi uhalifu unapojitokeza zisaidie kwenye upelelezi wa kuwabaini wahusika