Uturuki imethibitisha vifo 2,379 huku Syria ikirekodi vifo zaidi ya 1,400. Shirika la Afya Ulimwenguni, WHO linakadiria kuwa yumkini waliokufa ni mara nane zaidi ya idadi inayojulikana hivi sasa.
Wizara ya Afya ya Uturuki imesema kuwa magari ya kubebea wagonjwa yapatayo 813 yamepelekwa katika maeneo yaliyoathirika, na vikundi maalumu vya huduma za dharura zaidi ya 220 vimeambatana na magari hayo.
Tetemeko lenye ukubwa wa 7.8 kwenye kipimo cha Richter liliitikisa sehemu ya katikati mwa Uturuki na kaskazini mwa Syria alfajiri ya jana, na kufuatiwa na jingine dakika 10 baadaye, likiharibu vibaya miundombinu katika miji ipatayo 12.
