Mmoja wa wananchi walioathiriwa na mvua
Wananchi wa Kijiji hicho wanasema wanashangaa mvua hiyo kunyesha kwani haijawahi kutokea katika maisha yao huku, Mbunge wa jimbo la Lupembe Edwin Swale akilazimika kutoa msaada wa mabati 100 ili kuwanusuru wananchi waliokosa makazi.

Mazao yaliyoharibiwa
Aidha wananchi hao wameiomba serikali kuwasaidia msaada wa chakula na makazi ambapo Katibu Tawala wilaya ya Njombe amefika kijijini hapo na kujionea hali halisi ilivyo huku akiwaahidi wananchi hao kusaidiwa haraka iwezekanavyo.
