Saharat Sawangjaeng, alikamatwa wiki iliyopita huko Bangkok. Polisi, ambao walikuwa wakimsaka kijana huyo mwenye umri wa miaka 25 kwa miezi mitatu, walisema hana sura yake ya awali . Walimfuatilia kwa kufuatilia usambazaji wa dawa hizo kwa wauzaji wengine na wanunuzi huko Bangkok.
Walioshuhudia walimtaja kama mtu mwenye muonekano mzuri wa Kikorea . Pia alikuwa amebadilisha jina lake kuwa la Kikorea. Katika video ya kukamatwa kwake iliyotolewa na polisi, Bw Saharat alisema anataka kuhamia Korea Kusini na kwamba amechoka kuishi Thailand.
Bw Saharat ameshtakiwa kwa kuingiza dawa za kulevya kinyume cha sheria. Alikiri kuagiza MDMA - ambayo pia inajulikana kama ecstasy







