Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yapeleka msaada wa chakula Malawi

Saturday , 18th Mar , 2023

Jumla ya Tani 1000 za unga wa mahindi zimetolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni miongoni mwa misaada mbalimbali ya kibinadamu kwa nchi ya Malawi iliyoathiriwa na kimbunga Freddy ili kuisaidia nchi hiyo kukabiliana janga hilo

Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ), Luteni Kanali Gaudentius Ilonda

Hayo yamebainishwa Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ), Luteni Kanali Gaudentius Ilonda, amesema serikali imetoa misaada ya vitu mbalimbali ikiwemo chakula, mahema, na misaada mingine ya kibinadamu na Jeshi hilo ndilo litakalohusika kusafirisha misaada hiyo.

 

"Misaada iliyotolewa ni pamoja na Tani 1000 za unga wa mahindi (Tani 90 kutokea Dodoma na Tani 60 Iringa kuingia Malawi kila siku), Mablanket 6000, na mahema yasiyopungua 50".

Ilonda amesema magari ya JWTZ zaidi ya 37, yataondoka Dodoma muda wowote kuanzia hivi Sasa kupeleka misaada hiyo nchini Malawi.

"Baadhi ya magari hayo yanayopelekwa Malawi ni pamoja na Gari la wagonjwa(Ambulance), Karakana ya magari inayotembea(mobile workshop) na Malori makubwa ishirini yenye uzito wa Tani 30, na malori 10 yenye uzito wa Tani zaidi ya kumi na nane(18), pamoja na Helikopta mbili.

Mnamo Machi 13, mwaka huu kimbunga kiitwacho 'Tropic Freddy' kikiambatana na mvua kubwa na upepo mkali kiliikumba nchi ya Malawi kikisababisha vifo vya mamia ya watu na uharibu wa miundombinu.

Serikali imewatoa hofu wananchi, waonapo shehena ya magari yanayovuka mipaka pamoja na Helikopta kuelekea Malawi zisilete taharuki.

 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja