
Mwendesha mashtaka katika masuala ya haki za binadamu Sara Irene Herrerias amesema uchunguzi unafanyika juu ya tuhuma za mauaji na uharibifu wa mali.
Uchunguzi unaendelea juu ya wanaume watatu waliovaa sare walioonekana kwenye video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii wakishuhudia tukio hilo bila kuchukua hatua yoyote wakati moto ukiendelea kuwaka.
Awali Rais wa Mexico Andrés Manuel López Obrador, alitaja chanzo cha moto huo kuwa ni wahamiaji waliochoma moto magodoro baada ya kusikia watarejeshwa kwenye mataifa yao.