Friday , 28th Apr , 2023

Zaidi ya nyumba 50 zimeingia maji katika eneo la Bondeni lililopo Magomeni Makanya kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha katika Jiji la Dar es salaam na kusababisha hofu ya kupata magonjwa ya milipuko miongoni mwa wananchi wanaoishi katika eneo hilo

Wakizungumza na #EATV wakazi hao ambao wengine maji yameingia mpaka ndani ya nyumba hizo wamesema chanzo ni kuwepo kwa mto mdogo kwenye makazi yao ambapo mvua inaponyesha  maji yamekuwa  yakitirika katika mto huo badala ya kwenda moja kwa moja mto Ng"ombe

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Magomeni Makanya Chano Chano amesema wananchi hao wamekuwa wakiishi kwa hofu na wasiwasi mkubwa kila mara mvua inaponyesha 

Naye diwani wa kata ya Ndugumbi ambaye ndie anayesimamia eneo hilo Thadei Masawe ameeleza mpango wa halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni uliopo kwa sasa katika kuliendeleza eneo hilo Ili lisiendelee kuathiri makazi ya watu kwa maji kuingia kwenye nyumba zao