Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rc Chalamila aigeukia migogoro ya ardhi Dar.

Sunday , 2nd Jul , 2023

Mkuu wa Mkoa wa Dsm Albert Chalamila amewataka wananchi wa Mtaa wa Mbopo kata ya Mabwepande dsm ambao walivamia na kujenga Makazi yao katika Ardhi inayomilikiwa Kihalali na Shirika la Maendeleo la Mkoa wa Dsm DDC kutokubali kudanganywa na baadhi ya wanasiasa au Wanasheria wababaishaji

Mkuu wa Mkoa wa Dsm Albert Chalamila akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Mbopo kata ya Mabwepande.

Chalamilka ametoa kauli hiyo katika Mkutano uliofanyika katika Mtaa wa Mbopo ambapo amesema baadhi ya watumishi wa Umma hasa katika kitengo cha ardhi katika manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na baadhi ya wevyeviti wa Serikali za Mitaa hawakuwa waadilifu kwa kuuza na kutoa hati juu ya Ardhi yenye hati.

Katika Mkutano huo baadhi ya wananchi wamesema katika Kipindi kirefu walikuwa wakiishi kwa Mashaka kutokana na tishio la kubomolewa nyumba zao kutokana na kesi zote walizofungua mahakamani kushindwa lakini wakafarijika baada ya DDC kukaa nao na kuweka Mpango wa maridhiano na Kupimiwa ili kila Mwananchi alipe kigogo kidogo katika eneo analolimiliki.

Hata hivyo Chalamila alihitimisha Mkutano huo kwa kuwataka wananchi hao kuwa wakweli na kujiepusha na Makundi yanayowapotosha na kujipatia fedha na kuweka rehani Maisha yao badala yake wakubaliane na Mpango wa maridhiano na Shirika hilo kwa kupimiwa na kulipia ardhi kwa gharama kidogo ili Waendelee kuishi katika makazi yao.

 

 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi