Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sita (6) wakamatwa, mauaji ya mwanamuziki AKA

Wednesday , 28th Feb , 2024

Polisi nchini Afrika Kusini jana Jumanne wamesema kuwa wamewakamata watu sita wanaohusika na mauaji ya aliyekuwa Rapa maarufu Kiernan Forbes, maarufu kama AKA mnano Februari 2023.

Mwanamuziki huyo aliyefariki akiwa na umri wa miaka 35, alipigwa risasi na kuuawa yeye na rafiki yake Tebello "Tibz" Motshoane, Februari 10, mwaka jana wakati wakitembea nje ya mgahawa maarufu mjini Durban. AKA alipanga kutumbuiza katika klabu moja ya karibu usiku huo.

Kamishna wa Polisi, Nhlanhla Mkhwanazi amewafahamisha wanahabari kwamba "msimamizi, watu wawili wenye silaha, watekaji wawili, na mwingine aliyehusika na magari wakati wa tukio, wote watafikishwa mahakamani".

Inasemekana kuwa rapa huyo alikuwa akifuatwa kimya kimya tangu alipowasili katika uwanja wa ndege wa Durban hadi alipofika mgahawani.

Afrika Kusini ni miongoni mwa mataifa yenye viwango vya juu vya mauaji duniani, na mastaa kadhaa wa muziki nchini humo wameathirika na mauaji hayo.

Itakumbukwa mwaka 2007, Mwimbaji wa muziki wa Reggae Lucky Dube alipigwa risasi mara tatu wakati akimpeleka mtoto wake wa kiume katika nyumba ya jamaa yake.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi