Mwamuzi Issa Sy
FAF limetoa wito kwa CAF kumpiga marufuku mwamuzi wa Senegal Issa Sy na kumuondoa kwenye michuano hiyo mara moja.
Algeria ilipoteza 2-0, kwa mabao ya Victor Osimhen na Akor Adams, na hivyo kuhitimisha kampeni ya mbweha wa Jangwani. Mechi hiyo ilimalizika kwa fujo na mabishano yaliyohusisha Wachezaji na viongozi, pamoja na jaribio la kuvamia uwanjani.
CAF inasema imefungua uchunguzi na kupeleka kesi hiyo kwenye bodi yake ya Nidhamu.


