Waziri Mkuu aipa siku 2 Wizara ya Jafo
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ameipa siku mbili Wizara ya TAMISEMI kufuatilia halmashauri za wilaya ambazo zilikuwa na makao makuu yake katika halmshauri za miji, kuhakikisha zinahamia kwenye makao mapya na zisipotekeleza apelekewe taarifa ofisini kwake Jumamosi Februari 6 saa 4 asubuhi.