"Nawashangaa wanaosema Gambo simpendi "- Magufuli
Mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi, (CCM), Dkt. John Magufuli, amesema kuwa anawashangaa watu wanaopanda majukwaani na kusema kuwa yeye hampendi aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, na ndiyo maana alimfukuza kazi hiyo.