Aliyeachiwa kwa msamaha adakwa kwa Wizi Chalinze
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, amesema kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo linamshikilia Mustafa Malimi (25) ambaye juzi Desemba 9, 2019 alipata msamaha wa Rais Magufuli na kuachiwa huru kwa kosa la kuiba Ng'ombe mwenye thamani ya Shilingi milioni 1.2.