Waziri Mkuu ataka ibada zijenge jamii njema
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewaomba viongozi wa dini nchini wakiwemo wa Jumuiya ya Kiislamu ya Istiqaama Tanzania waongeze juhudi katika kutoa mafunzo ya dini ili kupunguza au kuondoa kabisa mmomonyoko wa maadili unaoikabili jamii.