Jumamosi , 10th Aug , 2019

Watu wanaokadiriwa kufika au zaidi ya 50 wamepoteza maisha baada ya kuungua na moto kufuatia Lori la mafuta kulipuka eneo la Msamvu mjini Morogoro. 

Sehemu ya athari za ajali hiyo

 

Lori hilo lilipata ajali majira ya saa 1:00 Asubuhi, ambapo Mkuu wa mkoa wa Morogoro Kebwe Stephen, amefika eneo la tukio na kuthibitisha kuwa miili ambayo imeshahesabiwa ni 54 huku mingine ikiendelea kutolewa katika eneo la ajali.

Mh Kebwe ameongeza kuwa baadhi ya majeruhi wamekimbizwa katika hospitali tofauti tofauti kwaajili ya huduma ikiwemo za macho kutokana na mafuta kuwaharibu macho na wengine kujeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwili.

UPDATES