Jumatano , 5th Apr , 2023

Mtu mmoja anayekadiriwa kuwa umri kati ya miaka 25-35 ambaye majina yake bado hayajatambulika amekutwa amefariki na kisha mwili wake kutupwa chini ya daraja la njia ya treni maeneo ya Bene barabara ya Iringa Manispaa ya Morogoro.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Morogoro Alex Mkama amethibisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mtu huyo amekutwa umeuawa huku mwili ukiwa umechomwa na kitu chenye ncha kali maeneo ya kifuani.

Kutokana na tukio hilo Kamanda Mkama amesema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi huku mtuhumiwa akitafutwa na mara baada ya kupatikana na upelelezi kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi.

Mbali na tukio hilo pia Kamanda Makama amesema katika maeneo ya Msamvu Manispaa ya Morogoro jeshi hilo limeokota miili miwili ya watoto (mapacha) ambao imetokana na kutolewa kwa  mimba ambayo haijafikia umri na kisha kutupwa eneo la karibu na kituo cha mabasi msamvu.