
Nyumba iliyosombwa na maji
Baadhi ya wakazi wa mtaa huo wamesema vifo hivyo vimetokea kwa kuwa bibi na wajukuu zake walikuwa wakiishi pembezoni mwa mto na kuiomba serikali kuwaondoa baadhi ya wanachi ambao nao wamejenga ndani ya eneo hilo la mto ili kuepusha vifo vingine kutokea.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto mkoa wa Mara Agustino Magere, amewataja waliofikwa na umauti huo kuwa ni Ghati Mwita 63 pamoja na wajukuu zake wawili ambao ni Jonson Denis miaka 10 na Violet Denis miaka 3
Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee, amefika katika eneo la tukio na kujionea hali halisi kisha akatoa maagizo kwa mkuu wa wilaya kufanya uchunguzi kama kuna watu wanaoishi kando ya mto huo waondolewe na kufutiwa hati zao.