Ijumaa , 28th Jan , 2022

Watu wawili wamepoteza maisha na wengine nane (8) kujeruhiwa, hii leo Januari 28, 2022, katika ajali iliyohususha lori na watembea kwa miguu maeneo ya Kimara Suka Jijini Dar es salaam, baada ya dereva wa lori hilo kupita kwenye kivuko cha watembea kwa miguu bila kuchukua tahadhari.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro

Taarifa ya ajali hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, na kusema kuwa ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa dereva wa lori ambaye amekimbia baada ya kusababisha ajali hiyo.

Aidha Kamanda Muliro, amesema kuwa majeruhi wote katika ajali hiyo walikimbizwa katika hospitali ya Bochi.