
Rais Magufuli akitoka Ikulu pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt.John Kijazi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega
Januari 15, Waziri Kigwangalla alialikwa na Rais Magufuli kufanya mazungumzo Ikulu Jijini Dar es salaam, lakini mshangao wa wengi ni katika picha alipokuwa akitoka nje na Rais Magufuli, iliyoonesha kiatu chake kikiwa na vumbi kali lililoziba rangi ya kiatu hicho.
Mwenyewe amesimulia namna mazingira yalivyokuwa hadi kupelekea kiatu chake kufunikwa na vumbi ilhali alikuwa ameitwa na Rais Ikulu.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Kigwangalla ameandika kuwa.
Nimevaa zangu jeans na shati nasafiri kwenda field Mikumi National Park; ghafla wito wa Ikulu, natupia kaunda suti ya dharura, kucheki sina moka, kuna mabuti/sneakers na siwezi kuhangaika kununua mpya, nkapiga buti nikaitika wito ndani ya muda! #RealMenWearBoots #MzeeWaField pic.twitter.com/OyF60qYf9L
— Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) January 17, 2019
Pia wakati akitoka kufanya mazungumzo na Rais Magufuli Ikulu, sambamba na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt.John Kijazi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega, Katibu Mkuu TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamuhanga, aliandika.
IKULU, Mapema leo: Mhe. RAIS: Hongera, naona unataka kwenda Zanzibar...umepata? KIGWANGALLA (akicheka): Ahsante Mhe., si unaona ni ‘keupe’? Mhe RAIS (akicheka): Tena wewe si unaruhusiwa wanne? KIGWANGALLA: Kabisa Mhe., bado nina nafasi tatu! pic.twitter.com/Rp5zKaHWzm
— Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) January 15, 2019
Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.