
Meya Iraqhe anabainisha kuwa kumekuwa na taarifa za upotoshaji katika mitandao kuhusu hali ya mapato katika jiji hilo, jambo ambalo sio sahihi ambapo anasisitiza kuwa hawatasita kumchukulia hatua za kisheria kwa atakaebainika anafanya hivyo
Katika hatua nyingine Iraghe anatoa angalizo kwa watumishi wanaofanya vitendo vya ubadhirifu fedha za miradi mbalimbali ikiwemo ya afya na elimu ambayo imewekwa kwa manufaa ya wananchi
Haya yanajiri ikiwa jiji hilo limefanikiwa kukusanya mapato ya ndani kwa kipichi cha Robo ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2022-2023 shilingi billion saba nukta tano tisa nane ikiwa ni ongezo la zaidi ya bilioni moja nukta tatu