Taarifa kutoka ikulu imesema kuwa Bi Anna Mghwira ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Taifa anaenda kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadick aliyekubaliwa kujiuzulu na Mh. Rais tar 16 Mei mwaka huu.
Pamoja na hayo Rais Magufuli amefanya uteuzi wa Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor, pamoja na DIGP Abdulrahman Omar Juma Kaniki kuwa Mabalozi na kwamba tarehe ya kuapishwa itatangazwa.
Barua ya uteuzi kutoka Ikulu.