
Profesa Mkenda, amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa maonyesho hayo ya bidhaa kutoka nchini Misri ambayo pamoja na mambo mengine yana lengo la kuvutia uwekezaji hapa nchini.
Kwa upande wao wafanyabiashara waliokuja kuonyesha bidhaa zao katika maonesho hayo wamesema kuwa wamevutiwa sana na mazingira ya kibiashara nchini hivyo wanahitaji ushirikiano wa pamoja na wafanyabiashara wa ndani ili waweze kufanya biashara pamoja.