
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Pili wa Kenya Daniel Arap Moi
Taarifa za kifo hicho zimetangazwa alfajiri ya leo Februari 4, 2020 na Rais Uhuru Kenyatta, ambapo Moi amekuwa akiugua kwa muda na mara kwa mara amekuwa hospitalini, licha ya kuwa mwenye afya nzuri baada ya kipindi chake cha Urais.
Kwa niaba ya Serikali na Watanzania nakupa pole Mhe.Rais Uhuru Kenyatta na Wakenya wote kwa kuondokewa na Rais Mstaafu Daniel Toroitich arap Moi. Watanzania tutamkumbuka kwa uongozi wake mahiri, jitihada za kuimarisha uhusiano wetu na Kenya na kufufua Jumuiya ya Afrika Mashariki.
— Dr John Magufuli (@MagufuliJP) February 4, 2020