Ijumaa , 14th Oct , 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameziagiza taasisi za TAKUKURU NA ZAECA kuhakikisha wanaendelea na uchunguzi wa miradi yote iliyobainika kuwa na dosari wakati wa ukaguzi wa Mwenge, ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Rais Samia ameyasema hayo leo wakati wa maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge  Mkoani Kagera, huku pia akizitaka taasisi hizo zenye  dhamana ya kuzuia na kupambana na rushwa pia kujichunguza pia.

“Vyombo tulivyoviamini TAKUKURU NA ZAECA kabla hamjaenda kushughulikia taasisi nyingine  naomba mjipekue ndani kwenu kwanza“ - Amesema Rais Samia Suluhu Hassan

Aidha Rais Samia amewataka watanzania kuendelea kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere kwa kufanya yale aliyoyahimiza na kuyaacha yale aliyokuwa akiyapinga ikiwa pamoja na vitendo vya rushwa na ufisadi.

Kwa takribani siku 195 Mwenge wa Uhuru umekagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 1293 yenye thamani ya shilingi bilioni 650.8 ambapo miradi ya setka ya maji imetajwa kufanya vizuri kuliko miradi ya sekta nyingine katika utekelezaji wake.