Ijumaa , 30th Dec , 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meneja Jenerali Suleiman Mzee amewaonya wakandarasi na wasimamizi wa miradi kushindwa kukamilisha miradi kwa wakati kwa kisingizio cha ugonjwa wa Uviko-19 jambo ambalo linapelekea miradi mingi kushindwa kukamilika kwa wakati

Kauli hiyo ameitoa wakati alipotembelea miradi wa maji wa Mgango, kiabakari, Butiama miradi   ambao ulitakiwa kukamilika mwezi huu wa desemba lakini mpaka sasa mradi huo upo asilimia 70 za utekelezaji wake huku mkandarasi mshauri akitupiwa lawama za kuwa chanzo cha ucheleweshwaji wa mradi huo

Akizungumiza mradi huo wa maji Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Mgango, kiabakari, Butiama amesema ujenzi huo umesogezwa mbele kutokana na kuchelewa kwa pampu za kusukuma maji toka ziwani kwenda katika matanki 


Mradi huo wa maji unategemea huhudumia zaidi ya wakaazi laki moja ndani ya vijiji  16 kwa awamu ya kwanza na utakapokamilika utafikia jumla ya vijiji 39 mkandarasi anaetekeleza mradi huu ni kampuni ya Unik Costaraction kutoka nchini Lethoto.