
Watatu wanaotuhumiwa kumuua bodaboda
Watuhumiwa hao wamefikishwa mahakamani leo Novemba 28, 2022, baada ya jitihada ya Jeshi la Polisi Kiteto kufuatilia mawasiliano yao toka awali kabla ya mauaji hayo.
Watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo Oktoba 21, 2022, ambapo baada ya kutekeleza mauaji yao walinyofoa viungo hivyo vya mwili wake.
Shtaka hilo limetajwa na watuhumiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uezo wa kusikiliza kesi hiyo na kesi imeahirishwa hadi Desemba 12, 2022.